Apo awali nilielezea ufugaji wa kaa na niliishia kwenye utengenezaji wa chakula cha kaa,napenda twendwe sambamba kutokea tulipoishia,kama wewe aujazisoma basi usijali zote zipo unaweza kuzitafuta kwa kupitia ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝhttps://profileofficial21.blogspot.com
Tunahitaji kutambua hakuna jambo lisilo na changamoto,na changamoto KUJITOKEZA ili uweze kuboresha.Ufagaji wa kaa ambao unategemea mazingira ya fukwe ya bahari inapelekea kujitokeza mambo kadhaa!
Aina ya chakula cha kutengeneza nichokielezea awali๐๐พkinawasaidia kaa kukomaa ndani ya wiki 3-5 wanakua na uzito wa kutosha na wanakua wamejaza nyama yaani wako vema Sana,sasa tuendelee๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ๐๐ฝ
CHANGAMOTO ZINAZOJITOKEZA KWENYE UFUGAJI WA KAA
1.Upatikanaji wa mbegu *Kaa maji*,ili uzalishaji wa kana wengi uongezeke ni muhimu kuwe na upatikanaji wa kutosha wa kaa maji ili wahifadhiwe kwenye cages kwa muda na wakomae waiingie sokoni.
2.Usafi wa vizimba wa kila siku,changamoto inajitokeza hasa pale unapokua na idadi kubwa ya vizimba vya kuvifanyia usafi,ili usafishe kizimba ni muhimu kaa aliye ndani yake umtoe kwanza ufanye usafi alafu umrejeshee kunahita umakini mkubwa
3.Ukosefu kwa wafanyakazi wenye ujuzi,endapo utakosa watu wenye ujuzi au utaalamu wa ufugaji au wenye uwezo wa kukamata na kumfunga kaa ni tatito kubwa Sana,kwasababu hautoweza kuwavuna wala kuwasafirisha,wafanyakazi wenye utaalamu wanjua namna ya kuwakamata ili wasivunjike na wanaweza kuwafunga vizuri
4.Vifo vya kaa,unapofuga vifo vya kaa vinajitokeza hasa vipindi vya joto,pia mbegu nyingi zinapokua na majeraha wanapelekea vifo kuwa vingi,ushauri unapokusanya mbegu wale kaa wenye majeraha watenganishe cages zao ili iwe lahisi kufagilia maendeleo tao
5.Wizi wa kaa shambani,unapoamua kufuga kaa Basi akikisha unaweka ulinzi kwenye eneo lako,kaa ni mali kilo moja ya kaa mkubwa yapata Tsh 7000-9000/= kwahiyo weka ulinzi endapo mtu atakuibia 12pcs tu ni sawa umepoteza Tsh 100000/=,Weka ulinzi usiku na mchana kaa ni mali Sana.
6.Kukatikakatika kwa miguu,kutokana na mazingira ya usafi kuhamisha hamisha au kung'atana inapelekea kukatika na kua reject endapo kaa amekatika thaman yake ya soko inashuka yapata Tsh 1500-3000/= na ndio maana unahitaji uwe na watu wenye kujua kukamata na kufunga vizuri
7.Keji kufumuka,endapo vizimba vinakua eneo ambalo linafikiwa zaidi na mawimbi inachangia cages kuhalibika na kaa wanatoka wenyewe kuingia baharini,zingatia unapojenga cages weka eneo ambalo mikoko iko mwanzo wa bahari na shamba liwe nyuma kidogo ya mikoko ili hata kama kunatokea mawimbi yatapozwa na miti ya mikoko iliyo mbele.
8.Kaa kukaa muda mrefu shambani,endapo kaa wanakomaa ni muhimu uwatoe shambani,unapofuga tafuta soko likusaidie kuwauza kwa wakati pindi wanapo tu wanapokamaa ili kuepuka vifo na reject visivyo vya lazima.
NB: Unapofuga nashauri kufuga kaa kuanzia medium 500gm na Large 700gm wa ndio wenye soko kubwa zaidi.
Mada itaendelea.....................!